Tuesday, 12 June 2012

[wanabidii] GYMKHANA CLUB NANI AMEWAROGA

Kwenu  Viongozi  Gymkhana Club


Mndengereko  mmoja   alipata  kusema  kwa  lugha  yake "  Changes  are inevitable"    na  mhehe  fulani  akaongezea "  Changes  are  Painfully".  Lakini   Ukienda   darasani  Changes    zina  stages  zake  ili  uweze  kufanikiwa.  Inategemea  unatumia  aina  gani  ya  changes.  Wiki  iliyopita  nilitembelea  mahali  ambapo  ndio  msingi   wa mimi  kuwa  hapa   nilipo  nikakutana  na  vitu  vya  ajabu  sana.   Niliingia  Gymkhana  Club   nikaenda  mens bar   nikakuta  wahudumu  tu  hakuna  hata member  mmoja. Nikaenda  kwa manji (Restaurant)  nikamkuta  amelala  na hakuna  watu  kabisa.  Ikabidi  niulize   Jamani  kulikoni.   Ndio  nikaambia  kuna  mabadiliko  ndugu  uongozi  mpya  na mambo  mapya.  Sikujali  sana  ila  kitu  kilichoniuma  ni  kufukuza   watoto  wa  wafanyakazi na  wanafunzi  wa  shule  mbali mbali   ambao  walikuwa   kwenye  training  mbali mbali   kama  za  golf  na  tennis kisa   sio  members.
Wakati  Captain  Malinzi anaingia  mwaka  2006   alikuta   Tanzania  ina  Golf  Professional  Wawili tu  Salim  Mwanyenza  na   Juma Mrami.  na wa  tatu  alikuwa  ni Davis  ambaye  yeye  alikuwa  based  sana  Mombasa.  Hivyo  Captain Malinzi  Akaanza  na Program  za kutrain  vijana   na  mpaka  anaondoka  madarakani  amecha professional   zaidi  ya  kumi.  Hawa professional  wote  ninaowasema  ni  watoto  wa  maskini  au  Caddies  hakuna  mtoto  wa  tajiri hata  mmoja. Ma pro  wengi  wa  golf   east  , southern  and  central    africa  ni macaddy  by  origin.  Nenda  south africa, zimbabwe  na  sehemu  yoyote  unayoijua    Caddies  ndio   professional  wa  Golf   Sehemu mbali  mbali  duniani  baada  ya  kuwa  promoted  kutokana  na  mashindano  mbali mbali  na uwezo  wanaouonyesha.  Ma  pro  wote  wa  tz  walikuwa  macaddy .   Sasa  leo  hii  kuwafukuza  wanafunzi  na   watoto  maana yake  unataka  mchezo  wa  golf  na tennis   uendelee  kuitwa  wa wazungu  na  matajiri tu. Ilichukua  miaka  mingi   golf  na tennis  ( Gymkhana  Club)  kuwa  club  ya  weusi   ilikuwa  ni ya  wahindi   na  wazungu  tu  mswahili  alikuwa   mr george  christos.  Alipoingia  Retired  Lietenant  G  Sayore  akaanza  kubadilisha  mchezo  wa  golf  kutoka  uzungu  na uhindi   na kuwa  wa watu  weusi.  Alijitahidi  kuwaleta  viongozi  wengi  na   wakubwa  wengi  ambao ni  waswahili  kwani  kulikuwa  na  waswahili  wachache  sasa  wanaocheza  golf.   Kutokana na members   watoto  wao  wanacheza  golf  as  leisure   ukaandaliwa  mpango  kabambe  wa  kutayarisha  vijana ili wawe  wachezaji  wazuri  wa  baadae   yaani  Golf  junior  academy  ambayo  inaudhamini  kutoka  st Endrews  na  Kwa  watu  mbali  mbali  ambapo  washiriki  ni  watoto  wa wafanyakazi   na  wanafunzi  wa shule  mbali  mbali  za msingi  na  sekondari.  Sio golf  tu  tenis  na  creket  wana  juniors  academy   zote  zimepigwa  marufuku  kisa   wanaofundishwa  sio  watoto  wa  matajiri. 
Kali  kabisa   Hakuna  mtu  yoyote  hata  atoke  wapi  atakaye ruhusiwa  kuingia  club   mpaka  awe  na  mwenyeji    na  alipe  kiingilio  cha  shilingi  elfu  kumi.  Na  akitaka  kucheza  mchezo kama golf  lazima  awe  na  mwenyeji  pia  na alipe  green fee   Tshs  80,000 .  Achilia  mbali  vifaa  vya  golf  vya  kukodi  na  caddy fee.   Gymkhana  inapokea  wageni  mbali mbali  kwa ajiri ya  mchezo wa golf  na  tennis   mpano:  marubani wa  ndege  za  kimataifa;  watalii  na   maofisa  ubalozi  na  wengine  wengi  ambao  wanapenda   kucheza  michezo  pasipo  kuwa  members  kwa  kulipa  viingilio  na  kucheza  mchezo  wanaotaka.  Kwa   changes  hizi  mpya  Gymkhana imekuwa  Tupu   na  kimya.  Na  hicho   kinapelekea   waajiriwa  na   wasio  ajiriwa  ( macaddy)  kufa  njaa.  Ukiachilia  mbali   maendeleo  ya  club  sijui  nini hatima yake.  Msisahau  Gymkhana  ni  Non Profit  Organization.   Wasi  wasi  wangu  ni kuturudisha enzi  zile  za   gymkhana  ya wazungu   kila  race  na  bar  yao  na  choo chao.   Members  mko  wapi    tunaua  michezo   wakati  ndio  kauli  mbiu  ya  serikali  kwa michezo  kwa  watoto  na  vijana.  Mzee  andanenga  anamalizia  kwa  kusema"  Kila  unachotizama  ,  usione  ukadhani.  Usione  jicho  kutazama  ukafikiri  linaona"  .  Jamani   hii ni tafsiri  yangu  wakati  wengine   wanaenda  club  as leisure  wengine  ndo  watoto  wao  wanenda  shule  na  nyumbani sufulia  zinachafuka.

Wenu  

XAVERY  LANGA  KAPECHA  NJOVU
FORMER  CADDY

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

0 comments:

Post a Comment